Ad Code

FASIHI KWA UJUMLA

Fasihi kwa ujumla

KARIBU KWENYE DARASA LA FASIHI


YALIYOMO
  • MAANA YA FASIH NA UCHAMBUZI WA VIPERA
  • MAANA NA METHALI ZILIZOKUSANYWA
  • CHIMBUKO NA ASILI YA LUGHA YA KISWAHILI 
  •  

MAANA YA FASIHI NA UCHAMBUZI WA VIPERA VYAKE 

Williady, (2015) Fasihi ni tawi moja wapo la sanaa linalotumia lugha katika kuwasilisha ujumbe wa mdomo au wa maandishi.
Wamitila (2004) Fasihi ni sanaa inayotumia luha na ambayo hujishughulisha na binadamu pamoja na maisha yake na huathri, hugusa au huacha athari fulanina hupatikana katika umbo ambalo linatambuliwa na jamii Fulani.
Kwakuwa fasihi ni aina ya sanaa, ni vyema mwanafunzi akajua pia maana ya sanaa.
MAANA YA SANAA
(Williady: 2015) Sanaa ni ujuzi au ufundi wenye kuleta manufaa kwa uma.

UMBO LA SANAA.

Tunaposema umbo la sanaa tunamaanisha matawi yanayojenga sanaa. Matawi hayo nipamoja na;

·       Fasihi
       ·       Maonyesho
·       Ususi
  ·       Uhunzi
  ·       Ufumaji
 ·       Utarizi
     ·       Uchongaji
    ·       Ufinyanzi
   ·       Uchoraji
 ·       Muziki

AINA/ KUMBO/ TANZU ZA FASIHI
Katika kumbo ya fasihi na taaluma zake kuna aina kuu mbili za fasihi, ambazo ni;
1.   Fasihi Simulizi
2.   Fasihi Andishi

TOFAUTI KATI YA FASIHI SIMULIZI NA FASIHI ANDISHI
     I.            Namna ya uwasilishaji wake. Fasihi simulizi huwasilishwa kwa njia yam domo wakati fasihi andishi uwasilishwa kwa njia ya maandishi.
 II.            Mabadiliko. Fasihi simulizi huweza kupokea mabadiliko ya papo kwa papo wakati fasihi andishi hurekebishwa baada ya toleo jipya.
III.            Utendaji wake kwa hadhira na fanani. Hadhira na fanani katika fasihi simulizi huwa ni yakiutendaji, wasikilizaji wanaweza kuchangia mawazo kwa kutoa maoni, kuuliza maswali au kushadadia masimulizi ya fanani. Fasihi andishi  hadhira hawawezi kuchangia lolote.

IV.            Ukongwe. Fasihi simulizi niyazamani zaidi, ilianza wakati mwanadamu alipoanza kutumia mdomo katika mawasiliano. Fasihi andishi ilianza pindi maandishi yalipobuniwa.

 V.            Vidato na elimu. Fasihi simulizi haiitaji mtu ajue kusoma ama kuandika, inamuhitaji mtu mwenye uwezo wa kuzungumza. Fasihi andishi inamhitaji mtu anayejua kuandika na kusoma.

VI.            Umiliki. Fasihi simulizi inamilikiwa na jamii nzima wakati fasihi andishi humilikiwa na mwandishi aliyeandika na kupiga chapa kazi hiyo.

VII.            Idadi ya tanzu. Fasihi simulizi inatanzu nyingi zaidi kuliko fasihi andishi.

VIII.            Kuhifadhi. Hapo kale fasihi simulizi ilihifadhiwa kichwani, kwa sasa fasihi simulizi yaweza kuhifadhiwa katika vinasa sauti, kaseti na santuri. Fasihi andishi yenyewe huifadhi wake ni kwa njia ya maandishi.

IX.            Mwingiliano wa tanzu kwa kiasi. Fasihi simulizi huweza kuingiliwa kwa kiasi kikubwa na tanzu nzingine kama vile methali, vitendawili, nyimbo na nahau wakati fasihi andishi huweza kuingiliwa na tanzu nyingine kwa kiasi kidogo.

UFAFANUZI WA AINA ZA FASIHI.

1.Fasihi simulizi

Fasihi simulizi ni aina ya fasihi inayotumia mdomo na utendaji wa viungo vya mwili katika kuwasilisha maudhui ya fanani kwa hadhira iliyokusudiwa.

                             TANZU ZA FASIHI SIMULIZI
     I.            Hadithi
 II.            Uigizaji
III.            Ushairi
IV.            Semi

                                  VIPERA VYA HADITHI
·       Ngano
·       Vigano
·       Hekaya
·       Soga
·       Tarihi
·       Visa
·       Visasili
·       Shajara
·       Istiala
·       Michapo
·       Mbazi
                                 VIPERA VYA UIGIZAJI
·       Miviga
·       Michezo ya jukwaani
·       Majigambo
·       Utani
·       Vichekesho
·       Ngonjera
·       Ngomezi
·       Mazungumzo

                                    VIPERA VYA USHAIRI
·       Nyimbo
·       Maghani
·       Ngonjera
·       Mashairi
·       Tenzi
·       Tendi

                                    AINA ZA NYIMBO
·       Bembezi
·       Nyimbo za mapenzi
·       Nyiso
·       Nyimbo za jadi
·       Nyimbo za harusi
·       Nyimbo za watoto
·       Nyimbo za sifa
·       Nyimbo za kampeni
·       Nyimbo za maombolezo
·       Nyimbo za chombezi

                                      VIPERA VYA SEMI
·       Methali
·       Misimu
·       Lakabu
·       Nahau
·       Vitendawili
·       Utani
·       Misimu
·       Mafumbo
·       Masaguo
·       Mizungu
·       Misemo

MAJUKUMU / DHIMA ZA FASIHI SIMULIZI KATIKA JAMII
      i.            Kuelimisha
          ii.            Kuburudisha
iii.            Kusisimua
iv.            Ukombozi
                                                                              v.            Kutoa mwongozo kwa jamii
                             vi.            Kutunza amali za jamii(historian a utamaduni)
                          vii.         Kujuza na kuunganisha vizazi na vizazi
viii.      Kufundisha
              ix.            Kudumisha ushirikiano
                                         x.            Kukuza stadi za lugha

MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA KATIKA USIMULIZI WA HADITHI

Ili msimuliaji aweze kutongoa au kusimulia hadithi kwa usahihi inampasa awe na weledi wa kutosha juu ya mbinu za kusimulia hadithi. Mbinu hozo ni hizi;

A)Dhima na maudhui

Msimuliaji wa hadithi anapaswa kujua lengo kuu (dhima) la hadithi yake. Vilevile msimuliaji anapaswa kujua maudhui ambayo ni jumla ya mambo yote yanayopelekea hadithi kutiririka vizuri kwenye mkondo wake.

B)Msuko

Msuko wa matukio kwa jina jingine unafahamika kama muundo. Kipengele hiki cha muundo kinahusu mpangilio wa hadithi kuanzia mwanzo mpaka mwisho.

C)Kusisimua

Kusisimua ni mbinu inayovuta umakini kwa watu. Msimuliaji anaweza kutumia mbinu kadhaa zitakazo msisimusha msomaji, mbinu kama vile taharuki, miguno na kelele za kutisha.

D)Urudufishaji

Huu ni urudiaji rudiaji katika fasihi simulizi. Mara nyingi msimuliaji anashauriwa kurudia rudia maneno, falsafa, nahau au vitendawili vilivyobeba lengo kuu la hadithi yake.

E)Chombezo

Chombezo ni kipengele kidogo kinacho elezwa na mtambaji wa hadithi chenye lengo la kupunguza ukakasi ama ukalia ama vitisho vilivyotokana na maudhui ya hadithi Fulani.
F)Nyimbo
Nyimbo zina kazi nyingi katika masimulizi ya hadithi. Moja wapo ya matumizi hayo ni kama vile kuondoa uchovu kwa wasikilizaji, kuvuta usikivu, kuwakaririsha hadhira falsafa au lengo kuu la hadithi hiyo.
MAMBO MENGINE
a)   Utulivu kwa hadhira
b)  Ujenzi wa wahusika
             c)   Matumizi ya tamathali za semi
d)  Ujenzi wa taswira
  
2.FASIHI ANDISHI
Williady(2015) fasihi andishi ni aina ya fasihi inayowasilishwa kwa ustadi wa maandishi yenye kuleta maana.
Wamitila (2004) fasihi andishi ni sanaa inayowasilishwa kwetu kwa maandishi.
TANZU ZA FASIHI ANDISHI
1.   RIWAYA (NATHARI)
2.   USHAIRI (NUDHUMU)
3.   TAMTHILIYA (SANAA ZA MAONYESHO)
FANI NA MAUDHUI KATIKA FASIHI
Fani na maudhui katika fasihi ndio maumbo mawili makuu yanayobeba sanaa hii.
FANI
Fani ni ufundi unaotumiwa na msanii katika kufikisha ujumbe uliokusudiwa, fani sio ujumbe bali ni mfano wa kipaza sauti kinachotumika kufikisha ujumbe.
VIPENGELE VYA FANI
Fani inavipengele vingi, kila kipengele kina husika kipekee kwa kutofautiana na kipengele kingine. 

Vipengele vya fani ni pamoja na;
a)   Muundo.
 Kipengele hiki hutumiwa kueleza mpangilio wa kazi ya kifasihi. Kwa ufupi kwenye kipengele cha muundo tunaangalia umbo la kazi ya fasihi, mfano kazi yaweza kugawanywa katika sura mbalimbali, sura hizi ndizo ujenga muundo.
b)  Mtindo.
Williady (2015) mtindo ni mbinu za kipekee zinazomtofautisha msanii mmoja na mwingine. Mfano katika fasihi simulizi kipengele cha nyimbo hadhira inaweza kusikia wimbo kwa mara ya kwanza na kutambua wimbo huo umeimbwa na nani bila ya kuambiwa na mtangazaji, hii huweza kutokea pindi mwimbaji mashuhuri anayetumia mtindo wa peke yake katika sauti na mpangilio wa mashairi anapotoa wimbo mpya. Huu ndio huitwa mtindo.
Katika fasihi andishi mtindo unaweza kujitokeza kwa njia za kipekee za mtunzi katika matumizi ya lugha, methali na misemo, msuko na mpangilio wa vina na mizani katika ushairi.
c)   Mandhari
Williady (2015) Mandhari ni eneo au mazingira ya kweli au yakubuni ambayo hutumiwa na mwandishi katika kuwajenga wahusika na uhusika wao. 

d)  Matumizi ya Lugha

Williady (2015) Matumizi ya lugha ni ustadi wa msanii katika kutumia lugha itakayoleta mvuto kwa wasomaji au wasikilizaji wa kazi ya fasihi.

Katika kutumia lugha msanii lazima azingatie kipengele cha uteuzi wa maneno yanayoendana na hadhira yake, maneno hayo ndiyo yatakayoleta mfungamanisho katika ya msanii, hadhira na ujumbe uliokusudiwa.

e)   Matumizi ya tamathali za semi(usemi)

Williady (2015) Tamathali maanayake ni neon moja au kifungu cha maneno kilicho sukwasukwa na kufichwa maana.

Baadhi ya tamathali za semi katika Kiswahili ni pamoja na;
Tashibiha, sitiari, tafsida, tashihisi, chuku, kinaya,dhihaka, mbalagha,tabaini

f)    Mbinu nyingine za kisanaa

Hapa huwa na mchanganyiko wa mbinu kadhaa katika usimulizi na silazima mbinu hizo zitumike zote kwa wakati mmoja. Mfano wa mbinu hizo ni pamoja na;
                                                                                                                                   i.            Takriri 
                                                                                                                                ii.            Kuchanganya ndimi
           iii.          Tanakali sauti 

iv.            Taswira
   v.            Lakabu
             vi.            Nahau na misemo

e)   Wahusika

Williady (2015) wahusika ni viumbe hai au viumbe ambao si hai wanaobebeshwa majukumu na msanii ili kuwafikishia hadhira ujumbe uliokusudiwa.

MAUDHUI KATIKA FASIHI SIMULIZI

(williady: 2015) Maudhui ni jumla ya mawazo anayoyazungumzia msanii au mtunzi katika kazi ya fasihi.
Maudhui hujumuisha vipengele mbalimbali, kama vile;

     I.            Dhamira
 II.            Ujumbe
III.          Falsafa
IV.            Mafunzo
 V.               Migogoro
VI.            Mtazamo

TANBIHI: Kuna baadhi ya wataalamu wa lugha wanakiweka kipengele cha migogoro upande wa fani na kunabaadhi wanakiweka kipengele hiki upande wa maudhui. Mimi nakiweka upande wa maudhui kwa kuwa migogoro inabeba kwa kiasi kikubwa ujumbe kuliko ufundi.

I.                 DHAMIRA

Dhamira ni shabaha kuu ya mtunzi wa kazi ya fasihi. Shabaha hii ukusudiwa ni nani wakumlenga nayo. Msanii anaweza kuwalenga kimaudhui watoto, wanawake, wasomi au watu wote katika jamii. Shabaha hii yaweza kuandikwa au kutongolewa kwa mdomo ikiwa na lengo la kupongeza, kuhimiza, kushauri, kutoa taarifa na kukosoa.

II.             UJUMBE

Ujumbe ni mawazo yanayotokana na dhamira, mawazo haya yaweza kujitokeza waziwazi au kwa kificho.

III.         FALSAFA

Falsafa ni hekima hekima ya mtunzi. Mtunzi huamini kuwa  kupitia imani hii jamii inaweza kupata suluhisho la matatizo yanayowakabili. Kwa mfano shekhe Shaaban Robert aliamini kuwa kila mwanajamii akiwa na utu basi haki na upendo vitapatikana kirahisi.

IV.         MAFUNZO

Mafunzo ni nasaha anazotoa mtunzi ambazo huifundisha hadhira maadili Fulani. Maana ya mafunzo hutegemea namna hadhira inavyofasili nasaha hizo.

V.             MIGOGORO

Migogoro ni misuguano au mikinzano ama kutoelewana kati ya pande mbili au zaidi ndani ya kazi za fasihi.

                                  AINA ZA MIGOGORO

     I.            Mgogoro kati ya mtu na mtu
 II.            Mgogoro kati ya mtu na jamii
III.            Mgogoro kati ya jamii na jamii 
IV.            Mgogoro wa nafsi


VI. MTAZAMO

Mtazamo na jinsi mwandisi anavyotazama na kuyachukulia matukio katika ulimwengu na athari zake kwa wanajamii. Mfano waandishi wengi wa mashairi wanamtazamoa huu “Kuibuka kwa maovu mengi duniani kwasasa  ni matokeo ya binadamu kuasi dini.

Chapisha Maoni

0 Maoni